Tuesday, December 20, 2016

South African police fire Rubber bullets at Congo Embassy protesters

South African police fired rubber bullets on Tuesday at scores of protesters outside the Democratic Republic of Congo embassy (DRC) in Pretoria demanding President Joseph Kabila step down, a spokesman said.
Several protesters were wounded and seven were arrested for public order offences, provincial police spokesman Kay Makhubela said. Kabila's mandate as DRC president expired at midnight, with no elected successor in place.

Tuesday, December 13, 2016

Majambazi waiba dhahabu ya kilo 70 Ufaransa

Majambazi waliokuwa na silaha wameiba dhahabu ya kilo 70 nchini Ufaransa na kutoroka.
Majambazi hao wanne waliokuwa wameabiri magari mawili walishambulia gari la usalama lililokuwa likisafirisha dhahabu hiyo karibu na mji wa Lyon.
Walitumia gari moja kuziba barabara.
Kisha, walichukua dhahabu hiyo inayokadiriwa kwua ya thamani ya €1.5m ($1.6m; £1.3m), na kuipakia kwenye gari moja lao ambalo walikuwa wamepanga kulitumia kutoroka.
Baada ya hapo, waliwafungia walinzi wawili waliokuwa wanasafirisha dhahabu hiyo nyuma ya gari lao kabla ya kuteketeza gari ambalo walikuwa wamelitumia kufunga barabara.
Walinzi hao waliokolewa na maafisa wa polisi baada ya mtu aliyeshuhudia tukio hilo kuwapasha habari.
Wezi hao walitoroka upesi na kuacha moto uliokuwa kwenye gari waliloliwasha moto ukienea na kufikia magari mengine yaliyokuwa karibu ingawa muda mfupi baadaye wazima moto walifika na kuuzima.
Kisa hicho kilitokea katika barabara ya A6 inayounganisha Lyon na Paris.
Polisi wanawasaka wahusika.

Monday, December 12, 2016

MZEE WA UPAKO:Wanaoniandika vibaya kufariki kabla ya mwezi wa tatu

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako jana amesema waandishi wote wa habari wanaoandika habari za kumchafua, watakufa kabla ya kufika Machi 2017.
Kauli hiyo ameitoa ikiwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo, akijibu yale yaliyoandikwa katika vyombo vya habari kuhusu kumfanyia fujo jirani yake na kulewa.
“Kila mwandishi aliyeniandika vibaya, ikifika mwezi wa tatu akiwa hai, mimi naacha kuhubiri, nafunga virago nakwenda kuuza gongo, sasa Mungu ndiye ataamua kwamba ama niache kuhubiri mimi au wewe ufe …najua hata leo mko humu mmekuja na mnasikiliza tu,”alisema.
“Akisema Mungu uishi wewe basi, nakuwa sina namna, lakini sijawahi kumtumikia Mungu ambaye ananyamaza. Nilishakubaliana mimi na Mungu, mpango wa Mungu ndiyo mpango wangu, sasa wajiandae, mimi siyo Sheikh Yahaya, mmeingia choo cha kike, nasema ‘Mama yangu mzazi’ nitaacha kuhubiri, nitaacha kuhubiri ….mimi nina nguvu saaana,”alisema.
Hata hivyo baadaye mchungaji huo alishuka na kusema anamuachia Mungu wake ambaye atawahukumu kwa wakati wake.
“Lakini Mungu anasema tusihukumu, namuachia Mungu atawahukumu kwa wakati wake, haleluya, haleluya, Mungu awabariki sana."
Novemba 24, mitandao ya kijamii ilikuwa na picha zinazomuonyesha Mzee wa Upako akirushiana maneno makali na jirani huyo ambaye anasikika sauti.
Taarifa za kukamatwa kwa kiongozi huyo wa kiroho zilisambaa baada ya mwandishi wa habari, Happiness Katabazi aliyeshuhudia tukio hilo, kuandika kwa urefu kisa hicho na kusambaza kwenye mitandao ya kijamii.
Novemba 26, Mzee wa Upako kwa mara ya kwanza alisita kuzungumzia sakata hilo na badala yake akasema wanaomtuhumu waendelee kusema: “Sisemi, lakini siogopi kwenda jela mimi na kwa taarifa yao watashindana sana, lakini hawatashinda. Hii ni kama kumpiga chura teke.”
Novemba 28, pia Mchungaji huyo akajibu akisema maneno aliyotumia ambayo ni mshenzi, mpumbavu na mjinga siyo matusi kwani yameandikwa kwenye biblia na kwamba watu hao ndiyo walianza kumtukana yeye baada ya kuwauliza wanatafuta nini eneo la getini kwake.
Jana, mchungaji huyo aliwahakikishia waumini wake akisema waandishi walioandika kwa lengo la kumchafua watakufa kabla ya kufika Machi mwakani.
Katika mahubiri yake yaliyojengwa na msingi wa Biblia kutoka kitabu cha Samweli wa kwanza, sura ya 16, mstari wa saba, Mzee wa Upako aliyekaribishwa kwa nyimbo kadhaa ikiwamo ‘kusanya kusanya’ alisema yeye siyo mchungaji anayejikweza, lakini baadhi ya wachungaji wakubwa kutoka nje wamekuwa wakienda kuomba upako.
Pia, alisema hata Rais John Magufuli hakumuita yeye bali aliona kitu ndani yake na kubarikiwa kabla ya kumtembelea.