Saturday, August 15, 2015

Friday, August 7, 2015

JUSA: TUNAHESHIMU MAAMUZ YA LIPUMBA

Chama cha wananchi CUF kimetoa kauli juu ya kujiuzulu kwa alie kua mwenyekiti wa CUF taifa prof Ibrahim haruna Lipumba.
Kauli hiyo imetolewa na kaimu mkurugenzi wa habari,uenezi,na mawasiliano na Umma Mhe Ismail jussa ladhu,Imesema kwamba CUF imepokea taarifa hiyo na inaheshimu maamuzi yake pamoja na kuwahiidi wanachama kua CUF haitayumba
"Tunapenda kuwahakikishia wanachama na wapenzi wa CUF na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwamba chama hichi hakitayumba"
alisema Ismail jussa
Mhe ismail jussa amesema CUF itaendelea kumheshimu kwa utumishi wake mkumbwa ndani ya chama pamoja na kuthamini mchango wake katika ujenzi wa demkrasia katika nchi yetu.
Kuondoka kwa proffessa lipumba katika Safu ya uongozi wa Cuf kutaacha pengo kubwa hasa kipindi hichi ambacho tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu.
Proff lipumba ni miongoni mwa waazilishi wa umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) ambao utamsimamisha waziri mkuu wa zamani Mhe Edward lowassa kama mgombea wake.

Thursday, August 6, 2015

Ukawa, Ccm zagawanyika

Wakati sintofahamu ya nini hatma ya dk wilbroad slaa bado haijafahamika ndani ya chadema,leo umoja wa katiba ya wananchi wamepata pigo jingine baada ya Mmoja kati ya nguzo muhimu ya ukawa kujiengua. Profesor Ibrahim lipumba ambaye alikuwa mwenyekiti wa CUF kwa takriban miaka 10 na zaidi ameamua kujiondoa katika nafasi hiyo katika chama chake na kusema kuwa atabaki kuwa mwanachama wa kawaida kwasababu kadi yake ya chama inakwisha muda wake mwaka 2020. Akiongea na waandishi mjini Dar es salaam profesa amesema kuwa amejiondoa nafas yake kwasababu ya cjadema kukiuka misingi ya makubaliano yao na hapendi kuwa miongoni mwa watu watakaoshiriki dhambi ya kuwadhulumu watanzania. Jaya yanatokea siku kadhaa baada ya chadema kumtangaza Edward lowasa kuwa mgombea wake na wa ukawa.